KUMBARIKI MGONJWA
Kumbariki Mgonjwa:
Padri anapowatazama wagonjwa hospitalini au nyumbani bila
kuwapa Sakramenti, aweza kusema hivi:
P. Tumsifu Yesu Kristo.
W. Milele. Amina.
KWA MTU MZIMA
P. Bwana Yesu Kristo awe nawe ili akulinde.
W. Amina
P. Awe mbele yako ili akuongoze, awe nyuma yako ili
akuimarishe.
W. Amina
P. Akutazame, akutunze na akubariki
W. Amina
P. Yeye anayeishi na kutawala pamoja na Baba na Roho
Mtakatifu milele.
W. Amina.
P. Baraka ya Mungu Mwenyezi, ya Baba + na
ya Mwana naya Roho Mtakatifu ikushukie na kukaa kwako daima.
W. Amina
KWA WATOTO
Tuombe. Ee Mungu, umewapangia malaika na
wanadamu kazi zao kwa azimio la ajabu. Basi ukubali
kwa wema wako, wale wanaosimama daima mbele yako
mbinguni wakutumikie, wayalinde maisha ya mtoto huyu
hapa duniani. Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
W. Amina.
P. Baraka ya Mungu Mwenyezi, ya Baba + na ya
Mwana na ya Roho Mtakatifu ikushukie na kukaa kwako daima.
W. Amina.