13
1 âSiku hiyo, kutatokea chemchemi ya kuwatakasa dhambi na unajisi wazawa wa Daudi na wakazi wote wa Yerusalemu. 2 Wakati huo, nasema mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, majina ya vinyago vya miungu nchini nitayaondoa, wala hayatakumbukwa tena. Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondolea mbali pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu. 3 Mtu yeyote akijidai kuwa nabii, baba na mama yake waliomzaa watamwambia, âUnapaswa kufa kwa kuwa unasema uongo kwa jina la Mwenyezi-Munguâ. Na haohao wazazi wake watamchoma kisu akiwa anatabiri. 4 Siku hiyo, kila nabii atayaonea aibu maono yake anapotabiri. Hawatavaa mavazi ya manyoya ili kudanganya watu, 5 bali kila mmoja atasema, âMimi si nabii. Mimi ni mkulima tu; nimeimiliki ardhi tangu ujana wanguâ. 6 Na mtu akimwuliza mmoja wao, âVidonda hivi ulivyo navyo mgongoni vimetoka wapi?â Yeye atajibu, âVidonda hivi nilivipata katika nyumba ya rafiki zangu.ââ 7 Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: âAmka, ee upanga! Inuka umshambulie mchungaji wangu; naam, mchungaji anayenitumikia. Mpige mchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyosha mkono wangu, kuwashambulia watu wadhaifu. 8 Theluthi mbili za watu katika nchi zitaangamizwa; ni theluthi moja tu itakayosalimika. 9 Theluthi hiyo moja itakayosalia, nitaijaribu na kuitakasa, kama mtu asafishavyo fedha, naam, kama ijaribiwavyo dhahabu. Hapo wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema, âHawa ni watu wanguâ, nao watasema, âMwenyezi-Mungu, ndiye Mungu wetu.ââ