JUMAMOSI JUMA 28 LA MWAKA WA 2
MASOMO

SOMO Efe 1:15-23
Tangu nilipopata habari za Imani yenu katika bwana Yesu, na pendo lenu kwa watakatifu wote, siachi kutoa shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu, Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu awape ninyi roho wa hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, tumjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo ;na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo. Kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake;ulipotenda katika kristo alipomfufua katika wafu,akamwekea mkono wake wa kuume katika ulimwngu wa roho ; juu sana katika ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani na kila jina litajwalo wala si ulimwenguni humu tu bali katika ule ujao pia akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

WIMBO WA KATIKATI: Zab.8:1-6
1. Wewe Mungu Bwana wetu,
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao.

(K) Umemtawaza mwanao juu ya kazi za mikono yako

2. Nikiziangalia mbingu zako, Kazi ya vidole vyako,
Mwezi na nyota ulizoziratibisha,
Mtu ni kitu gani hat umkumbuke
Na binadamu hata umwangalie. (K)

3. Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu;
Umemvika taji ya utukufu na heshima
Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. (K)

SHANGILIO: Yn.14:5
Aleluya, aleluya!
Nakushukuru baba Bwana wa mbingu na nchi, Kwa kuwa mambo haya uliyaficha Wenye hekima na akili, Ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya!

INJILI: Lk.12:8-12
Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Nami nawaambia, kila atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri yeye mbele ya malaika wa Mungu; na mwenye kunikana mbele ya watu, huyo atakanwa mbele ya malaika wa Mungu. Na kila mtu atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali aliyemkufura Roho Mtakatifu hatasamehewa. Na watakapowapeleka ninyi mbele ya masinagogi na maliwali na wenye mamlaka, msifadhaike kwa kuwaza maneno yenu jinsi mtakavyojibu au kusema; kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha saa ile ile yawapasayo kuyasema.