5
1 Ee Yerusalemu, vua vazi lako la huzuni na mateso, ukavae milele uzuri wa utukufu wa Mungu. 2 Jivike joho la uadilifu utokao kwa Mungu; vaa kichwani taji la utukufu wa Mungu wa milele. 3 Maana Mungu atadhihirisha fahari yako kila mahali duniani. 4 Mungu atakupa jina hili milele: “Amani kwa uadilifu; fahari kwa uchaji wa Mungu.” 5 Inuka, ee Yerusalemu, usimame milimani, tazama upande wa mashariki, uwaone watoto wako wamekusanywa kutoka mashariki na magharibi, kwa amri ya Mungu Mtakatifu. Wanashangilia kwani Mungu amewakumbuka. 6 Waliondoka kwako kwa miguu, wakichukuliwa na maadui zako. Lakini Mungu atawarejesha tena kwako wakiwa wamebebwa kwa fahari kama juu ya kiti cha enzi cha mfalme. 7 Mungu ametoa amri: Milima na vilima visawazishwe, na mabonde yafukiwe, nchi yote iwe tambarare, Waisraeli watembee salama kwa utukufu wa Mungu. 8 Kwa amri ya Mungu, vichaka na miti itoayo harufu nzuri itawapa kivuli Waisraeli. 9 Mungu atawaongoza Waisraeli kwa furaha; kwa mwanga wa utukufu wake, kwa uadilifu utokao kwake mwenyewe.