101
Mwongozo mzuri wa mfalme(Zaburi ya Daudi) 1 Utenzi wangu kuhusu uaminifu na haki; ninauimba kwa heshima yako, ee Mwenyezi-Mungu. 2 Nitazingatia mwenendo usio na hatia. Je, utakuja kwangu lini? Nitaishi kwa unyofu nyumbani kwangu; 3 sitavumilia kamwe upuuzi. Nayachukia matendo ya watu wapotovu, mambo yao hayataambatana nami. 4 Upotovu wowote ule uwe mbali nami; sitahusika kabisa na uovu. 5 Anayemsengenya jirani nitamfutilia mbali; sitamvumilia mwenye majivuno na kiburi. 6 Nitawaangalia kwa wema watu walio waaminifu, wapate kuishi pamoja nami. Watu wanyofu ndio watakaonitumikia. 7 Mwongo yeyote hatakaa nyumbani mwangu; hakuna msema uongo atakayekaa kwangu. 8 Siku kwa siku nitawaangamiza waovu wote nchini; nitawaangamiza wabaya wote mjini mwa Mwenyezi-Mungu.