150
Zaburi ya kumsifu Mungu 1 Msifuni Mwenyezi-Mungu! Msifuni Mungu katika patakatifu pake; msifuni katika mbingu zake kuu. 2 Msifuni kwa sababu ya matendo yake makuu; msifuni kwa ajili ya utukufu wake mkuu. 3 Msifuni kwa mlio wa tarumbeta; msifuni kwa zeze na kinubi! 4 Msifuni kwa ngoma na kucheza; msifuni kwa filimbi na banjo! 5 Msifuni kwa kupiga matoazi. Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa. 6 Kila kiumbe hai kimsifu Mwenyezi-Mungu! Msifuni Mwenyezi-Mungu!