125
Usalama wa watu wa Mungu(Wimbo wa Kwenda Juu) 1 Wanaomtegemea Mwenyezi-Mungu, wako kama mlima Siyoni, ambao hautikisiki bali wabaki imara daima. 2 Kama Yerusalemu inavyozungukwa na milima, ndivyo Mwenyezi-Mungu awazungukavyo watu wake, tangu sasa na hata milele. 3 Waovu hawataendelea kutawala nchi ya waadilifu; wasije waadilifu nao wakafanya maovu. 4 Ee Mwenyezi-Mungu, uwe mwema kwa watu wema, kwa wale wanaozitii amri zako. 5 Lakini wanaogeuka na kufuata njia zao mbaya uwakumbe pamoja na watenda maovu. Amani iwe na Israeli!