122
Sifa za Yerusalemu(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi) 1 Nilifurahi waliponiambia: “Twende nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.” 2 Sasa tuko tumesimama, kwenye malango yako, ee Yerusalemu! 3 Yerusalemu, mji uliojengwa, ili jumuiya ikutane humo. 4 Humo ndimo makabila yanamofika, naam, makabila ya Israeli, kumshukuru Mwenyezi-Mungu kama alivyoagiza. 5 Humo mmewekwa mahakama ya hukumu ya haki, mahakama ya ukoo wa kifalme wa Daudi. 6 Uombeeni Yerusalemu amani: “Wote wakupendao na wafanikiwe! 7 Ndani ya kuta zako kuwe na amani, majumbani mwako kuweko usalama!” 8 Kwa ajili ya jamaa na ndugu zangu, ee Yerusalemu, nakutakia amani! 9 Kwa ajili ya nyumba ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ninakuombea upate fanaka!