120
Kuomba msaada(Wimbo wa Kwenda Juu) 1 Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu, naye akanijibu. 2 Uniokoe ee Mwenyezi-Mungu, na watu wadanganyifu na waongo. 3 Enyi watu wadanganyifu, mtapewa kitu gani? Mtaadhibiwa namna gani? 4 Kwa mishale mikali ya askari, kwa makaa ya moto mkali! 5 Ole wangu kwamba naishi kama mgeni huko Mesheki; naishi kama mgeni katika mahema ya Kedari. 6 Nimeishi muda mrefu mno kati ya watu wanaochukia amani! 7 Wakati ninaposema nataka amani, wao wanataka tu vita.