75
Mungu hakimu(Kwa Mwimbishaji: Mtindo āUsiharibuā. Zaburi ya Asafu. Wimbo) 1 Tunakushukuru, ee Mungu, tunakushukuru! Tunatangaza ukuu wa jina lako na kusimulia juu ya matendo yako makuu. 2 Mungu asema: āMimi nimeweka wakati maalumu! Wakati huo nitahukumu kwa haki. 3 Nchi ikitetemeka na vyote vilivyomo, mimi ndiye ninayeitegemeza misingi yake. 4 Nawaambia wenye kiburi: āAcheni kujigambaā; na waovu: āMsioteshe pembe za kiburi! 5 Msijione kuwa watu wa maana sana, wala kusema maneno ya majivuno.āā 6 Hukumu haitoki mashariki au magharibi; wala haitoki nyikani au mlimani. 7 Mungu mwenyewe ndiye hakimu; humshusha mmoja na kumkweza mwingine. 8 Mwenyezi-Mungu, anashika kikombe mkononi, kimejaa divai kali ya hasira yake; anaimimina na waovu wote wanainywa; naam, wanainywa mpaka tone la mwisho. 9 Lakini mimi nitafurahi milele, nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo. 10 Atavunja nguvu zote za watu waovu; lakini nguvu za waadilifu ataziimarisha.