124
Mungu kinga yetu(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi) 1 “Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu Semeni nyote mlio katika Israeli: 2 “Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu, wakati ule tuliposhambuliwa na maadui, 3 hakika tungalimezwa tukiwa hai, wakati hasira zao zilipotuwakia. 4 Tungalikumbwa na gharika, tungalifunikwa na mto wa maji, 5 mkondo wa maji ungalituchukua!” 6 Atukuzwe Mwenyezi-Mungu, ambaye hakutuacha makuchani mwao. 7 Tumeponyoka kama ndege mtegoni; mtego umeteguliwa, nasi tukaokoka. 8 Msaada wetu watoka kwa Mwenyezi-Mungu, aliyeumba mbingu na dunia.