20
Kuomba ushindi(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi) 1 Mwenyezi-Mungu akujibu uwapo taabuni; jina la Mungu wa Yakobo likulinde. 2 Akupelekee msaada kutoka hekaluni mwake; akutegemeze kutoka mlima Siyoni. 3 Azikumbuke sadaka zako zote; azikubali tambiko zako za kuteketezwa. 4 Akujalie unayotamani moyoni mwako, aifanikishe mipango yako yote. 5 Tutashangilia kwa ajili ya ushindi wako; tutatweka bendera kulitukuza jina la Mungu wetu. Mwenyezi-Mungu akutimizie maombi yako yote! 6 Najua Mwenyezi-Mungu atamsaidia mfalme aliyemteua, atamjibu kutoka patakatifu pake mbinguni; kwa mkono wake wa kulia atamjalia ushindi mkubwa. 7 Wengine hujigamba kwa magari ya vita; wengine hujigamba kwa farasi wao. Lakini sisi twajivunia Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu. 8 Hao watajikwaa na kuanguka; lakini sisi tutainuka na kusimama imara. 9 Umjalie mfalme ushindi, ee Mwenyezi-Mungu; utujibu wakati tunapokuomba.