129
Sala dhidi ya maadui wa Israeli(Wimbo wa Kwenda Juu) 1 “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu Kila mtu katika Israeli na aseme: 2 “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu, lakini hawakufaulu kunishinda. 3 Walinijeruhi vibaya mgongoni mwangu, wakafanya kama mkulima anayelima shamba. 4 Lakini Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu; amezikata kamba za hao watu waovu.” 5 Na waaibishwe na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia mji wa Siyoni. 6 Wawe kama nyasi juu ya paa la nyumba, ambazo hunyauka kabla hazijakua, 7 hakuna anayejishughulisha kuzikusanya, wala kuzichukua kama matita. 8 Hakuna apitaye karibu atakayewaambia: “Mwenyezi-Mungu awabariki! Twawabariki kwa jina la Mwenyezi-Mungu!”