141
Hatari za tamaa mbaya(Zaburi ya Daudi) 1 Nakuita, ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia! Uisikilize sauti yangu wakati ninapokuita! 2 Sala yangu uipokee kama ubani; niinuapo mikono yangu kwako unikubali kama tambiko ya jioni. 3 Ee Mwenyezi-Mungu ukilinde kinywa changu, uweke ulinzi mlangoni mwa mdomo wangu. 4 Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishughulishe na matendo maovu; nisijiunge na watu watendao mabaya, wala nisishiriki kamwe karamu zao. 5 Afadhali mtu mwema anipige kunionya; lakini sikubali kamwe kusifiwa na wabaya, maana nasali daima dhidi ya maovu yao. 6 Wakuu wao watakapopondwa miambani, ndipo watatambua maneno yangu yalikuwa sawa. 7 Mifupa yao itatawanywa mdomoni pa Kuzimu kama kuni zilizopasuliwa vipandevipande! 8 Bali mimi nakutegemea, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu; ninakimbilia usalama kwako, usiniache hatarini. 9 Unikinge na mitego waliyonitegea, uniepushe na matanzi ya hao watu waovu. 10 Waovu wanaswe katika mitego yao wenyewe, wakati mimi najiendea zangu salama.