98
Mungu mtawala wa dunia yote 1 Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu! Mkono wake hodari, mkono wake mtakatifu umempatia ushindi. 2 Mwenyezi-Mungu ameonesha ushindi wake; ameyadhihirishia mataifa uwezo wake wa kuokoa. 3 Amekumbuka fadhili na uaminifu wake kwa Waisraeli. Pande zote za dunia zimeuona ushindi wa Mungu wetu. 4 Dunia yote imshangilie Mwenyezi-Mungu; imsifu kwa nyimbo na vigelegele. 5 Msifuni Mwenyezi-Mungu kwa shangwe, msifuni kwa sauti tamu za zeze. 6 Mpigieni vigelegele Mwenyezi-Mungu mfalme wetu, mshangilieni kwa tarumbeta na sauti ya baragumu. 7 Bahari na ivume na vyote vilivyomo; dunia na wote waishio ndani yake. 8 Enyi mito pigeni makofi; enyi vilima imbeni pamoja kwa shangwe. 9 Shangilieni mbele ya Mwenyezi-Mungu, maana anakuja kutawala dunia. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, atawatawala watu kwa uadilifu.