131
Kumtumainia Mungu kwa utulivu(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi) 1 Ee Mwenyezi-Mungu, sina moyo wa kiburi; mimi si mtu wa majivuno. Sijishughulishi na mambo makuu, au yaliyo ya ajabu mno kwangu. 2 Ila nafsi yangu imetulia na kuwa na amani, kama mtoto mchanga alivyotulia na mama yake; ndivyo nafsi yangu ilivyo tulivu. 3 Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu, tangu sasa na hata milele.