KITABU CHA KWANZA(Zaburi 1–41) 1
Furaha ya kweli 1 Heri mtu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki njia za wenye dhambi, wala kujumuika na wenye dharau; 2 bali huifurahia sheria ya Mwenyezi-Mungu, na kuitafakari mchana na usiku. 3 Huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki. Kila afanyalo hufanikiwa. 4 Lakini waovu sivyo walivyo; wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo. 5 Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu, wenye dhambi hawatakaa na kusanyiko la waadilifu. 6 Maana Mwenyezi-Mungu huziongoza njia za waadilifu; lakini njia za waovu zitaishia katika maangamizi.