113
Sifa kwa Mungu mtukufu 1 Msifuni Mwenyezi-Mungu! Enyi watumishi wa Mwenyezi-Mungu, lisifuni jina lake! 2 Jina lake litukuzwe, sasa na hata milele. 3 Kutoka mashariki na hata magharibi, litukuzwe jina la Mwenyezi-Mungu! 4 Mwenyezi-Mungu atawala juu ya mataifa yote, utukufu wake wafika juu ya mbingu. 5 Nani aliye kama Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu? Yeye ameketi juu kabisa; 6 lakini anatazama chini, azione mbingu na dunia. 7 Humwinua fukara kutoka mavumbini; humnyanyua maskini kutoka unyonge wake, 8 na kumweka pamoja na wakuu; pamoja na wakuu wa watu wake. 9 Humjalia mwanamke tasa furaha nyumbani kwake; humfurahisha kwa kumjalia watoto. Msifuni Mwenyezi-Mungu!