137
Ombolezo ugenini 1 Kando ya mito ya Babuloni, tulikaa, tukawa tunalia tulipokumbuka Siyoni. 2 Katika miti ya nchi ile, tulitundika zeze zetu. 3 Waliotuteka walitutaka tuwaimbie; watesi wetu walitutaka tuwafurahishe: “Tuimbieni mojawapo ya nyimbo za Siyoni!” 4 Twawezaje kuimba wimbo wa Mwenyezi-Mungu katika nchi ya kigeni? 5 Ee Yerusalemu, kama nikikusahau, mkono wangu wa kulia na ukauke! 6 Ulimi wangu na uwe mzito, kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalemu; naam, nisipokuthamini kuliko furaha yangu kubwa! 7 Ee Mwenyezi-Mungu, usisahau waliyotenda Waedomu, siku ile Yerusalemu ilipotekwa; kumbuka waliyosema: “Bomoeni mji wa Yerusalemu! Ngoeni hata na misingi yake!” 8 Ee Babuloni, utaangamizwa! Heri yule atakayekulipiza mabaya uliyotutenda! 9 Heri yule atakayewatwaa watoto wako na kuwapondaponda mwambani!