47
Mungu, Mfalme wa ulimwengu wote(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Wakorahi) 1 Enyi watu wote, pigeni makofi! Msifuni Mungu kwa sauti za shangwe! 2 Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu Mkuu, anatisha. Yeye ni Mfalme mkuu wa ulimwengu wote. 3 Ametuwezesha kuwashinda watu wa mataifa, ameyaweka mataifa chini ya mamlaka yetu. 4 Ametuchagulia nchi hii iwe urithi wetu, ambayo ni fahari ya Yakobo anayempenda. 5 Mungu amepanda juu na vigelegele, Mwenyezi-Mungu na sauti ya tarumbeta. 6 Mwimbieni Mungu sifa, mwimbieni! Mwimbieni mfalme wetu sifa, mwimbieni! 7 Mwimbieni Mungu sifa kwa tenzi; maana yeye ni mfalme wa ulimwengu wote. 8 Mungu anayatawala mataifa yote; amekaa katika kiti chake cha enzi kitakatifu. 9 Viongozi wa watu wa mataifa wanakusanyika, wanajiunga na watu wa Mungu wa Abrahamu, maana nguvu zote duniani ni zake Mungu, yeye ametukuka sana.