3
Kuomba msaada asubuhi(Zaburi ya Daudi alipomkimbia Absalomu) 1 Ee Mwenyezi-Mungu, tazama walivyo wengi adui zangu, ni wengi mno hao wanaonishambulia. 2 Wengi wanasema juu yangu, “Hatapata msaada kwa Mungu.” 3 Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu u ngao yangu kila upande; kwako napata fahari na ushindi wangu. 4 Nakulilia kwa sauti, ee Mungu, nawe wanisikiliza kutoka mlima wako mtakatifu. 5 Nalala na kupata usingizi, naamka tena maana wewe ee Mwenyezi-Mungu wanitegemeza. 6 Sitayaogopa maelfu ya watu, wanaonizingira kila upande. 7 Uje ee Mwenyezi-Mungu! Niokoe ee Mungu wangu! Wewe wawavunja mataya maadui zangu wote; wawavunja meno waovu wasinidhuru. 8 Mwenyezi-Mungu ndiwe uokoaye; uwape baraka watu wako.