121
Mungu kinga yetu(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi) 1 Natazama juu milimani; msaada wangu utatoka wapi? 2 Msaada wangu watoka kwa Mwenyezi-Mungu, aliyeumba mbingu na dunia. 3 Hatakuacha uanguke; mlinzi wako hasinzii. 4 Kweli mlinzi wa Israeli hasinzii wala halali. 5 Mwenyezi-Mungu ni mlinzi wako; yuko upande wako wa kulia kukukinga. 6 Mchana jua halitakuumiza, wala mwezi wakati wa usiku. 7 Mwenyezi-Mungu atakukinga na baya lolote; atayalinda salama maisha yako. 8 Mwenyezi-Mungu atakulinda katika shughuli zako zote tangu sasa na hata milele.