23
Mungu mchungaji wangu(Zaburi ya Daudi) 1 Mwenyezi-Mungu ni mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. 2 Hunipumzisha kwenye malisho mabichi; huniongoza kando ya maji matulivu, 3 na kuirudishia nafsi yangu nguvu mpya. Huniongoza katika njia sawa kwa hisani yake. 4 Nijapopita katika bonde la giza kuu la kifo, sitaogopa hatari yoyote, maana wewe ee Mwenyezi-Mungu u pamoja nami; gongo lako na fimbo yako vyanilinda. 5 Umeniandalia karamu mbele ya maadui zangu; umenipaka mafuta kichwani pangu; kikombe changu umekijaza mpaka kufurika. 6 Kweli wema wako na fadhili zako zitakuwa pamoja nami, siku zote za maisha yangu; nami nitakaa nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu milele.