87
Sifa ya Yerusalemu(Zaburi ya Wakorahi. Wimbo) 1 Mungu amejenga mji wake juu ya mlima wake mtakatifu. 2 Mwenyezi-Mungu anaupenda mji wa Siyoni, kuliko makao mengine ya Yakobo. 3 Mambo ya fahari yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu: 4 “Miongoni mwa wale wanijuao mimi, wapo watu wa Misri na Babuloni. Kadhalika Filistia, Tiro na Kushi, wote walizaliwa kwako!” 5 Na kuhusu Siyoni itasemwa: “Siyoni ni mama wa huyu na huyu; Mungu Mkuu atauthibitisha.” 6 Mwenyezi-Mungu ataandika katika kitabu, atakapoorodhesha watu: “Huyu amezaliwa huko!” 7 Wote wanacheza ngoma na kuimba: “Siyoni, chanzo chetu ni kwako.”