136
Wimbo wa shukrani 1 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 2 Mshukuruni Mungu wa miungu; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 3 Mshukuruni Bwana wa mabwana; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 4 Ndiye peke yake atendaye makuu ya ajabu; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 5 Ndiye aliyeziumba mbingu kwa hekima; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 6 Ndiye aliyeitengeneza nchi juu ya vilindi vya maji; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 7 Ndiye aliyeumba jua, mwezi na nyota; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 8 Jua liutawale mchana; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 9 Mwezi na nyota vitawale usiku; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 10 Ndiye aliyewaua wazaliwa wa kwanza wa Misri; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 11 Akawaondoa watu wa Israeli kutoka huko; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 12 Kwa mkono wake wenye nguvu na enzi; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 13 Ndiye aliyeigawa Bahari ya Shamu sehemu mbili; kwa maana fadhili zake zadumu milele, 14 akawapitisha watu wa Israeli humo; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 15 Lakini akawazamisha humo Farao na jeshi lake; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 16 Ndiye aliyewaongoza watu wake jangwani; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 17 Ndiye aliyewapiga wafalme wenye nguvu; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 18 Akawaua wafalme maarufu; kwa maana fadhili zake zadumu milele; 19 akamuua Sihoni, mfalme wa Waamori, kwa maana fadhili zake zadumu milele; 20 na Ogu, mfalme wa Bashani; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 21 Akachukua nchi zao akawapa watu wake; kwa maana fadhili zake zadumu milele; 22 ziwe riziki ya Israeli, mtumishi wake; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 23 Ndiye aliyetukumbuka wakati wa unyonge wetu; kwa maana fadhili zake zadumu milele; 24 akatuokoa kutoka maadui zetu; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 25 Ndiye akipaye kila kiumbe chenye uhai chakula; kwa maana fadhili zake zadumu milele. 26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni; kwa maana fadhili zake zadumu milele!