8
Utukufu wa Mungu na cheo cha binadamu(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Gitithi. Zaburi ya Daudi) 1 Ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wetu, kweli jina lako latukuka duniani kote! Utukufu wako waenea mpaka juu ya mbingu! 2 Kwa sifa za watoto wadogo na wanyonyao, umejiwekea ngome dhidi ya adui zako, uwakomeshe waasi na wapinzani wako. 3 Nikiangalia mbingu, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizozisimika huko, 4 mtu ni nini, ee Mungu, hata umfikirie, binadamu ni nini hata umjali? 5 Umemfanya awe karibu kama Mungu, umemvika fahari na heshima. 6 Ulimpa madaraka juu ya kazi zako zote; uliviweka viumbe vyote chini ya mamlaka yake: 7 Kondoo, ng'ombe, na wanyama wa porini; 8 ndege, samaki, na viumbe vyote vya baharini. 9 Ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wetu, kweli jina lako latukuka duniani kote!