142
Dua ya mtu aliyeachwa mpweke(Utenzi wa Daudi alipokuwa pangoni. Sala) 1 Namlilia Mwenyezi-Mungu kwa sauti, namsihi Mwenyezi-Mungu kwa sauti yangu. 2 Namwekea malalamiko yangu, namweleza taabu zangu. 3 Ninapokaribia kukata tamaa kabisa, yeye yupo, anajua mwenendo wangu. Maadui wamenitegea mitego njiani mwangu. 4 Nikiangalia upande wa kulia na kungojea, naona hakuna mtu wa kunisaidia; sina tena mahali pa kukimbilia, hakuna mtu anayenijali. 5 Nakulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu! Wewe ni kimbilio langu la usalama; wewe ni riziki yangu kuu katika nchi ya walio hai. 6 Usikilize kilio changu, maana nimekuwa hoi; uniokoe na watesi wangu, maana wamenizidi nguvu. 7 Unitoe humu kifungoni, ili nipate kukushukuru. Watu waadilifu watajiunga nami kwa sababu umenitendea mema mengi.