110
Kutawazwa kwa mfalme mteule(Zaburi ya Daudi) 1 Mwenyezi-Mungu amwambia bwana wangu: “Keti upande wangu wa kulia, hata niwaweke maadui zako chini ya miguu yako.” 2 Mwenyezi-Mungu ataeneza enzi yako kutoka Siyoni; utatawala juu ya maadui zako wote. 3 Watu wako watakujia kwa hiari, siku utakapokwenda kuwapiga maadui. Juu ya milima mitakatifu watakujia vijana wako, kama umande unaotokeza alfajiri mapema. 4 Mwenyezi-Mungu amekuapia wala hatabadili nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.” 5 Bwana yuko upande wako wa kulia; atawaponda wafalme atakapokasirika. 6 Atayahukumu mataifa na kuwaua watu wengi; atawaponda viongozi kila mahali duniani. 7 Mfalme atakunywa maji ya kijito njiani; naye atainua kichwa juu kwa ushindi.