128
Tuzo kwa jamaa imchayo Mungu(Wimbo wa Kwenda Juu) 1 Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu, wanaoishi kufuatana na amri zake. 2 Utapata matunda ya jasho lako, utafurahi na kupata fanaka. 3 Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako; watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako. 4 Naam, ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Mwenyezi-Mungu. 5 Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni! Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako. 6 Uishi na hata uwaone wajukuu zako! Amani iwe na Israeli!