134
Msifuni Mungu(Wimbo wa Kwenda Juu) 1 Njoni kumsifu Mwenyezi-Mungu enyi watumishi wake wote, enyi nyote mnaotumikia usiku nyumbani mwake. 2 Inueni mikono kuelekea mahali patakatifu, na kumtukuza Mwenyezi-Mungu! 3 Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni; yeye aliyeumba mbingu na dunia.