126
Kuomba nguvu mpya(Wimbo wa Kwenda Juu) 1 Mwenyezi-Mungu alipoturekebisha na kuturudisha Siyoni, tulikuwa kama watu wanaoota ndoto! 2 Hapo tuliangua kicheko; tulishangilia kwa furaha. Nao watu wa mataifa mengine walisema: “Mwenyezi-Mungu amewatendea mambo makubwa!” 3 Kweli Mwenyezi-Mungu alitutendea mambo makubwa, tulifurahi kwelikweli! 4 Ee Mwenyezi-Mungu, urekebishe tena hali yetu, kama mvua inavyotiririsha maji katika mabonde makavu. 5 Wanaopanda kwa machozi, watavuna kwa shangwe. 6 Wanaokwenda kupanda mbegu wakilia, watarudi kwa furaha wakichukua mavuno.