126

Kuomba nguvu mpya
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1 Mwenyezi-Mungu alipoturekebisha na kuturudisha Siyoni, tulikuwa kama watu wanaoota ndoto!
2 Hapo tuliangua kicheko; tulishangilia kwa furaha. Nao watu wa mataifa mengine walisema: “Mwenyezi-Mungu amewatendea mambo makubwa!”
3 Kweli Mwenyezi-Mungu alitutendea mambo makubwa, tulifurahi kwelikweli!
4 Ee Mwenyezi-Mungu, urekebishe tena hali yetu, kama mvua inavyotiririsha maji katika mabonde makavu.
5 Wanaopanda kwa machozi, watavuna kwa shangwe.
6 Wanaokwenda kupanda mbegu wakilia, watarudi kwa furaha wakichukua mavuno.

Generic placeholder image