114
Mungu na watu wake 1 Watu wa Israeli walipotoka Misri, wazawa wa Yakobo walipotoka ugenini, 2 Yuda ikawa maskani ya Mungu, Israeli ikawa milki yake. 3 Bahari iliona hayo ikakimbia; mto Yordani ukaacha kutiririka! 4 Milima ilirukaruka kama kondoo dume; vilima vikaruka kama wanakondoo! 5 Ee bahari, imekuwaje hata ukakimbia? Nawe Yordani, kwa nini ukaacha kutiririka? 6 Enyi milima, mbona mliruka kama kondoo dume? Nanyi vilima, mmerukaje kama wanakondoo? 7 Tetemeka, ee dunia mbele yake Mwenyezi-Mungu; tetemeka mbele ya Mungu wa Yakobo, 8 anayeugusa mwamba ukawa bwawa la maji, nayo majabali yakawa chemchemi za maji!