61
Kuomba ulinzi(Kwa Mwimbishaji: Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi) 1 Ee Mungu, usikie kilio changu, usikilize sala yangu. 2 Ninakulilia kutoka miisho ya dunia, nikiwa nimevunjika moyo. Uniongoze juu kwenye mwamba mkubwa 3 maana wewe ndiwe kimbilio langu, kinga yangu imara dhidi ya adui. 4 Naomba nikae nyumbani mwako milele nipate usalama chini ya mabawa yako. 5 Ee Mungu, umezisikia ahadi zangu, umenijalia sehemu yangu unayowapa wale wakuchao. 6 Umjalie mfalme maisha marefu, miaka yake iwe ya vizazi vingi. 7 Atawale milele mbele yako, ee Mungu; fadhili na uaminifu wako vimlinde. 8 Hivyo nitakuimbia nyimbo za sifa, nikizitekeleza ahadi zangu kila siku.