82
Mungu mtawala mkuu(Zaburi ya Asafu) 1 Mungu anasimamia baraza lake; anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu: 2 “Mpaka lini mtaendelea kuhukumu bila haki na kuwapendelea watu waovu? 3 Wapeni wanyonge na yatima haki zao; tekelezeni haki za wanaoonewa na fukara. 4 Waokoeni wanyonge na maskini, waokoeni makuchani mwa wadhalimu. 5 “Lakini nyinyi hamjui wala hamfahamu! Nyinyi mnatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki duniani imetikiswa! 6 Mimi nilisema kuwa nyinyi ni miungu; kwamba nyote ni watoto wa Mungu Mkuu! 7 Hata hivyo, mtakufa kama watu wote; mtaanguka kama mkuu yeyote.” 8 Inuka ee Mungu, uuhukumu ulimwengu; maana mataifa yote ni mali yako.