70
Kuomba msaada(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi ya matoleo ya ukumbusho) 1 Upende kuniokoa ee Mungu! Ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia. 2 Wanaonuia kuniangamiza, na waaibike na kufedheheka! Hao wanaotamani niumie, na warudi nyuma na kuaibika. 3 Hao wanaonisimanga, na wapumbazike kwa kushindwa kwao. 4 Lakini wote wale wanaokutafuta, wafurahi na kushangilia kwa sababu yako. Wapendao wokovu wako, waseme daima: “Mungu ni mkuu!” 5 Nami niliye maskini na fukara, unijie haraka, ee Mungu! Ndiwe msaada wangu na mkombozi wangu; ee Mwenyezi-Mungu, usikawie!